Masomo
ya Kumbukumbu ya Kuingia Bwana Yerusalemu kwa Shangwe
Mk
11:1-10 au Yn 12:12-16
Somo
I. Isa. 50:4-7, Somo la II. Flp 2:6-11, Inj. Mk 14:1-15,47
Kanisa leo
linaadhimisha dominika ya matawi ya mateso. Ni dominika ya matawi kwasababu
tunakumbuka kuingia Bwana Yerusalemu kwa
shangwe ambako alishangiliwa na watu kwa kutikisa matawi ya mitende akiwa
amepanda punda. Tunafanya kumbukumbu hiyo kwa kubariki matawi na kuingia
kanisani kwa maandamano tukiongozwa na padre anayemwakilisha Kristu na kutikisa
matawi yetu tukiimba hosanna mwana wa
daudi. Dominika hii huitwa ya mateso pia kwa sababu inatuingiza kwenye wiki kuu
ambamo tunaadhimisha mateso kifo na kuzikwa kwa Bwana wetu Yesu Kristu. Kumbukumbu
ya kuingia kwa Bwana Yerusalemu kwa shangwe ikiishia tu kuwa ishara ya nje haitakuwa
na umuhimu kwetu kwa hiyo ni vema basi tukatakafakari juu ya maana ya ishara
hiyo ili dhimisho la leo lizae matunda ndani yetu.
Tukio la Bwana kuingia
Yerusalem kwa shangwe laonesha ujasiri wa Yesu wa kuyakabili mateso yake
mwenyewe kwa ajili ya ukombozi wetu. Yesu anaingia Yerusalem wakati saa yake
ikiwa imefika yaani muda muafaka wa kukamatwa, kuteswa na kuuawa kwa ajili ya ukombozi wetu. Yesu akijua
haya yote na ya kwamba yatatokea Yerusalem, walipo wakuu wa mahukani na
mafarisayo waliowaka hasira na chuki dhidi yake; wakitafuta nafasi ya kumkamata
kwa udi na uvumba, anaingia Yerusalemu kwa uwazi akiwa amepanda punda
akijionesha mbele ya umma wa watu bila kuogopa watesi wake. nay a kwambahaya
yote yatatokea Yerusalem. Katika hali ya kawaida ya mwanadamu Yesu angeingia
Yesrusalem kwa siri na kujificha ili watesi wake wasimuone au pengine wapate
shida kidogo katikaa kumtafuta. Lakini yesu anawarahisishia kazi kwa kuingia
kwa uwazi. Anatufundisha ujasiri katika kupokea mateso ambayo hayaepukiki
katika maisha yetu kwa ajili ya kutimiza mapenzi ya Mungu
Kumbukumbu ya kuingia Yerusalemu
kwa shangwe inatufundisha kuwa daima tumtafute Yesu kwa ajili ya wongofu ili
tuwe tayari kumfuata katika hali zote za raha na taabu. Tusimfuate na kumkimbilia
Yesu kwa sababu ya kuvutwa na uwezo
wake wa kufanya miujiza au mambo yasiyokuwa ya kawaida, umahiri wake wa
kuhubiri au kwa ajili ya kutimiza
malengo ya ubinafsi wetu. Kati ya watu waliokuwa wanamshangilia Yesu walikuwepo
wengi waliomfuata kwa sababu walimuona akitenda miujiza mingi na hasa walivutwa
na muujiza kwa kumfufua Lazaro kule Betania. Kwa ujumla wake pia wayahudi wengi
walimshangilia Yesu wakidhani kuwa yeye ni masia wa kisiasa anakuja kuuupindua
utawala wa Kirumi kwa mtutu ili awarudishie utawala wao. Hawakumshangilia Yesu
kwa sababu ni Masiya anayekuja kuwatoa kwenye utawala wa dhambi. Kwa sababu ya
malengo hayo potofu ndio maana watu wote waliomshangilia ndio waligeuka kuwa
maadui wake pale msalabani
Tunaalikwa leo tuwe
tayari kufungua mioyo yetu ili tusikie sauti ya Mungu na tujifunze mapenzi yake
kwetu. Yesu daima amekuwa akiwafundisha watu ili waelewe kuwa yeye ni nani hasa
na amekuja duniani kwa ajili ya kazi gani . Lakini kutokana na ugumu wa mioyo
ya watu na hasa kwa sababu ya ubinafsi
hawakuwa tayari kusikia. Daima walibaki na mtazamo wao wa masia wa kisiasa. Kabla
ya kuingia kwenye saa yake Yesu anafanya jitihada ya mwisho ya kuwafungua macho
Wayahudi ili waelewe aina ya masiya anayewajia
kwa kufanya ishara ya nje, mbinu ilizotumiwa
na manabii waliomtangulia ili kuwafanya Wayahudi walelewe ujumbe wa Mungu baada ya kushindwa
kwa maneno, unaweza kurejea (1Fal
11:30-2). Kwa kawaida Huko Palestina punda ni mnyama mwenye hadhi kubwa sana. Ni
mnyama anayetumiwa na mfalme wakati wa amani. Kukiwa na vita mfalme hutumia
farasi. Yesu anaamua kuingia Yerusalemu kwa shangwe akiwa amepanda punda ili
awafundishe kuwa yeye ni mfalme na masia lakini ni mfalme wa amani na upendo na
wala si mfalme wa vita. Pamoja na kufanya hayo yote Wayahudi walishindwa kumuelewa
kwa sababu mioyo yao ilifungwa na ubinafsi wao. Nasi tukiruhusu ubinafsi wetu
ututawale hatutatoa nafasi ya kusikiliza sauti ya Mungu inayoutuelekeza
kutimiza mapenzi yake.
Kristu anapoamua kupanda
punda kama ishara ya mfalme wa amani anatufundisha kuwa silaha bora ya kupambana na
adui ni upendo, huruma na amani. Wayahudi walikuwa na adui ambaye ni utawala wa
Kirumi uliwofanya kuwa koloni lao. Walimsubiria mkombozi atakayekuja kumshinda
adui huyu na kumtoa kwa upanga ili
awarudishie utawala wao, lakini kwa kupanda punda Yesu anawaambia kuwa yeye ni
Mkombozi anayekuja kupambana na adui kwa kumpa upendo na uhuruma ili adui huyu aguswe dhamiri yake na abadilike kuwa mtu mwema.
Wayahudi waliimba hosanna mwana wa Daudi wakimaanisha utuokoe
kutoka lugha ya kiebrania. Kama ambavyo tumeona hapo awali, wokovu walioutarajia
wayahudi kutoka kwa Yesu ni wokovu wa kisiasa yaani Yesu awaongoze katika vita
ya kuwaondosha Warumi katika nchi yao na kuwapatia uhuru. Sisi tunapoimba leo hosanna
mwana wa Daudi tunamuita Yesu atuokoe kwanza kiroho yaani atuongoze
katika vita ya kumng’oa Shetani katika roho zetu na kutupatia uhuru wetu wa roho
ili tuwe na amani na furaha. Lakini
zaidi ya hapo tukisha okoka ndani yetu , Yesu atuokoe katika mifumo dhalimu ya
kisiasa, kiuchumi na kijamii inayowafanya watu wateseke kwa kukosa chakula,
malazi, afya bora, elimu na haki nyingine nyingi za binadamu
Tumuombe Mungu ili
dominika ya leo ituingize vyema katika tafakari ya mateso na kifo cha Bwana
wetu Yesu Kristu tusije tukafanana na wale
wa wayahudi ambao walimshangilia lakini muda mfupi baadae walimgeuka. Tufanane na
mama bikira Maria na yule mwanafunzi, waliolewa maana ya Kristu kuteseka na
wakakubali kuteseka pamoja naye ili wapate wokovu.
No comments:
Post a Comment