Mdo 1:15-17, 20a, 20c-26,
I Yoh 4:11-16, Inj. Yn 17:11b-19
Wakristu tunao uhakika kuwa kiongozi wetu Yesu Kristu hata baada ya kupaa
kwake mbinguni anaendelea kuwa pamoja nasi kutuongoza, kutuimarisha, kutubariki
katika safari yetu ya kuelekea kule aliko yeye. Kwa mara nyingine leo
tunakumbushwa kuwa ukristu wetu unatudai mambo makubwa sana yanayohitaji
kujitoa mhanga kwa ajili ya Kristu kiongozi wetu. Peke yetu hatuwezi ni lazima
tuombe msaada wake kwa njia ya sala yeye aliyetuahidi kuwa pamoja nasi mpaka
mwisho wa safari.
Katika njili Yesu kuhani mkuu
analiombea kundi lake kabla ya kuteswa, kufa, kufufuka na kupaa kwake mbinguni.
Katika sala ya Yesu tunaweza pamoja na mambo mengi tukatafakri mambo makubwa
manne kuhusu ukristu wetu.
Mkristu safi, hodari na shujaa si
yule anayejitenga na ulimwengu bali yule anayeishi ndani ya ulimwengu lakini
anaushinda ulimwengu. Yesu haombi kwamba tutoke ulimwenguni bali tulindwe na
yule mwovu. Mara nyingi nimesikia watu mbalimbali walio katika ndoa wanawaambia
mapadre na watawa kuwa afadhali wao wamechagua maisha ya kujitenga na ulimwengu
kwa kuwa watawa au mapadre kwani wameepukana na maouvu ya
ulimwengu. Ingawaje si kweli kwamba mapadre na watawa wametoka katika ulimwengu
huu lakini hoja ya watu wanaofikiri hivyo kuhusu mapadre ni kwamba mtu atakuwa
mkristu mzuri kama atatoka katikati ya ulimwengu uliojaa maovu jambo ambalo si
la kweli. Wapendwa maisha ya ukristu maana yake ni kwenda kinyume na ulimwengu
huo huo tunaoishi. Tunapaswa kuwa mashuhuda wa Kristu, kwa mfano, katika
ulimwengu unaotumia mitandao ya kijamii kubomoa maaadili kwa sisi kutumia
mitandao hiyo vizuri na si kuacha kutumia. Ukristu hautuweki huru dhidi ya
matatizo bali unatupa mbinu za kupambana na matatizo
Wakristu tumewekwa wakfu yaani
tumetengwa kwa ajili ya kazi maalumu. Sehemu ya mwisho ya sala ya kristu katika
injili ya leo yaeleza ukweli huu Kristu anapoomba tutakaswe na hiyo kweli. Tumezoea
kuwa mapadre na watawa tu ndio wamewakwa wakfu lakini ukweli ni kwamba kwa
ubatizo wetu sisi sote tumetengwa kwaajili ya kazi maalumu ya kumshuhudia Kristu
popote ulimwenguni kwa maneno na matendo yetu. Ni kweli kwamba mapadre na
watawa wamewekwa wakfu kwa namna ya pekee lakini hili halifuti ukweli kuwa kila
mbatizwa amewekwa wakfu kuwa shahidi wa Kristu. Kila mkristu popote alipo
anapaswa kutambua kuwa yeye ni mteuliwa wa Kristu, ametengwa kwa ajili ya
kumtambulisha Kristu kwa watu kwa utakatifu wake. Unapokuwa shuleni, sehemu ya
kazi, nyumbani unapaswa kutambua kuwa wewe umechaguliwa na Kristu kuwa mfano wa
maisha ya utakatifu, kinyume cha hapo unakufuru kwa kutenda uovu.
Silaha ya kumshinda mwovu hapa
duniani ni kwa wakristu kuwa na umoja. Ni kwa bahati mbaya sana kati ya vitu
ambavyo Kristu aliliombea kanisa lake umoja wa wakristu umepata misukosuko
mingi. Wakristu wanapaswa kuwa na roho moja na moyo mmoja katika Kristu. Wapo
watu katika ulimwengu huu ambao wanatumia silaha ya utengano kwa wakristu ili
kujinufaisha katika mambo yao. Tumeona mara kadhaa wanasiasa wanavyovuruga
kanisa ili likose msimamo mmoja katika kutetea maadili mema na hivyo wapate
nafasi ya kukanyaga haki za watu kwa manufaa yao binafsi.
Wakristu tuna uhakika wa ulinzi
wa Kristu dhidi ya mwovu tukiwa ulimwenguni. Yesu anatulinda kwa kweli ili
tusiingie katika mtego wa shetani wa kutenda dhambi. Ulinzi huu tutaupata ikiwa
tutakuwa tayari kuutafuta. Mara kadhaa kumekuwa na maswali inakuwaje watu wasio
na hatia wanateseka na kufa kutokana na makosa ya watu wengine ikiwa Kristu
anatuombea kwa Baba ili tulindwe na huyo mwovu. Si rahisi sana kusema kwa
uhakika kwa nini haya yanatokea kwa sababu mateso bado ni fumbo kwetu. Lakini sisi
wakristu daima tunaalikwa kumuangalia Kristu kiongozi wetu ambaye aliishi kila
kitu sawa na sisi isipokuwa hakutenda dhambi, na bado akafa kifo cha aibu
msalabani. Ufufuko wake umedhihirisha kuwa mateso ya mwili kwa mkristu si kitu
ikiwa ameishi akiwa anamwamini Kristu. Hivyo pale inapotokea watu wasio na
hatia wanateswa na kufa na wakati mwingine
kwa sababu ya imani yao, hatupaswi kumlaani Mungu kwa kudhani kuwa Mungu hayupo
au hatupendi.
Somo la kwanza latutafakarisha
juu ya wajibu wetu wa Kikristu. Katika kumchagua mtu atakayekuwa mbadala wa
Yuda Iskariote wakristu wakwanza waliongozwa na neno hili kuwa anapaswa awe
shahidi wa ufufuko wa Kristu. katika somo hilo tunaelezwa jinsi ambavyo kanisa
letu lenye watu zaidi ya bilioni leo hii lilikuwa na watu 120 tu wakati Matiya
anachaguliwa kuwa mbadala wa Yuda. Inaonesha jinsi gani wakristu wa kwanza
walifanya kazi kubwa ya kushuhudia ufufuko wa Kristu kiasi cha mimi na wewe leo
kuitwa wakristu na huo ndio wajibu wetu mkuu kama wakristu.
Uhusiano wetu na Kristu umejengwa
katika msingi wa upendo, hivyo ndivyo anavyotuambia Yohane katika somo la pili.
Mungu ni upendo, kwa upendo wake ametuumba, ametukomboa, anaendelea kututegemeza
na atatupa tuzo ya urithi wa mbingu milele. Kila tunapopendana tunakaa ndani ya
Mungu, tunamualika Mungu kati yetu na Mungu anakaa ndani yetu. Upendo wa Mungu
unajidhihirisha katika unyenyekevu. Ni rahisi sana mtu kuonesha unyenyekevu kwa
mtu aliye mkubwa wake, kiumri ama kicheo au yule aliye na vipaji vingi kumzidi.
Hebu fikiri ilivyo ngumu kwa mtu kujinyenyekesha kwa mdogo wake kiumri ama
kicheo au kwa mtu aliyemzidi katika elimu ama vipaji na karama mbalimbali. Hivi
ndivyo Mungu alivyotupenda, yeye aliyekuwa Mungu akatwaa hali ya utumwa ili
atutumikie sisi viumbe vyake
Ikiwa kila mkristu ataona kuwa
maisha ya hapa duniani ni maandalizi tu ya maisha mazuri na yenye raha mbinguni,
itakuwa ni motisha tosha ya kupambana siku hadi siku ili kufikia maisha hayo. Tuombe kwa Mungu ili
daima tutafute kuwa mashuhuda wake kwa maneno na matendo yetu ili kufikia
ukamilifu anaoutegemea kwetu.
Online blackjack table game - Ozlemgultekin
ReplyDeleteOnline blackjack table game - 4 player online blackjack. Free spins - bonus round; 바카라 사이트 쿠폰 Free spins - 안전 바카라 사이트 bonus round; Free spins - bonus round; Free spins - bonus round; Free spins - bonus 실시간 바카라 사이트 round; 넥스트 바카라 Free spins - bonus round; Free spins - bonus round; Free spins - bonus round; Free 온라인 바카라 사이트 spins - bonus round; Free spins - bonus round; Free spins - bonus round;