Friday, 10 April 2015

DOMINIKA YA PILI YA PASAKA MWAKA B. APRIL 12, 2015

Somo I. Mdo 4:32-35, Somo II. IYn 5:1-6, Injili Yn 20:19-31
Fadhila ya imani ni kushawishika kwa moyo na kweli za KiMungu bila kutegemea tu ushahidi wa  milango yetu ya fahamu. Ufufuko wa Yesu ni ushindi dhidi ya kifo cha mwili na cha roho. Ushindi huu unatuingiza katika maisha mapya ya furaha milele, maisha yasioyoonja taabu ya aina yeyote ile milele yote. Furaha hii ya milele tutaipata kikamilifu mara ya baada ya kumaliza maisha yetu ya hapa duniani. Furaha hii inapita furaha zote za ulimwengu huu. Pamoja na kwamba hatujawahi kuipata furaha hiyo lakini tuamimi kwamba ipo na tutaipata.

Imani ya Tomaso kwa Yesu Mfufuka  kadiri ya  injili ya leo inategemea tu ushahidi wa milango ya fahamu. Baada tu ya kumuona Tomaso anamkiri kuwa Bwana wake na Mungu wake na kuanzia hapo anapata tamanio la kuungannika na Kristu huyu mfufuka na anaishi kadiri ya tamanio hilo hadi kufa shahidi. Hatuoni kwamba Kristu amestaajabishwa sana na imani ya Tomaso baada ya ungamo lake. Badala yake Kristu anawabariki wale wote wanaotamani kuunganika na Kristu kwa kusikia tu habari zake kutoka kwa watu wengine na sauti ya dhamiri zao bila ya kumuona wala kugusa madonda yake. Kristu ni kama vile anamwambia Tomaso ikiwa kila mtu atakayefuata baada ya yeye kwenda mbinguni akahitaji kumuona na kugusa madonda yake  ili amwamini hata baada ya kuhubiriwa, hakutakuwa na waaamini kwani hawatapata nafasi ya kumuona na kumgusa Kristu.

Katika somo la kwanza, Wakristu wa kanisa la kwanza walishawishiwa juu ya  ufufuko wa Kristu kwa mahubiri ya mitume peke yake bila kuhitaji kumuona wala kumgusa Kristu. Ufufuo wa Kristu ulibadilisha mtazamo wao. Uliwafanya  waamini kuwa maisha ya Mbinguni yana raha zaidi kuliko raha za dunia hii zinazotokana na mali ingawaje hawajawahi kuishi mbinguni. Tamanio hili la maisha ya raha ya Mbinugni liliwafanya waone kuwa si tatizo kwao kufanya kila kitu shirika, kila mtu kutoa mali zake kwa ajili ya maihitaji ya jumuiya.

Neno la Mungu katika somo la pili linatueleza kuwa imani yetu kwa kristu, Mungu kweli na mtu kweli, inatufanya tuushinde ulimwnegu. Kristu aliyekubali kuwa mtu alionja upinzani mkali kutoka ulimwengu huu, nguvu kama vile mateso, uchungu, umasikini, ubinafsi, mali,  zinazotaka ufalme wa Mungu usienee duniani. Yesu mtu kweli alishinda vita dhidi ya nguvu zote hizi pinzani na daima alikuwa mtii kwa mapenzi ya Mungu. Yeyote anayemwamini Kristu Mungu kweli na mtu kweli, aliyeshinda upinzani wote huu katika ubinadamu wake daima atauushinda ulimwengu katika nguvu zake zote pinzani dhiidi ya mapenzi ya Mungu.


Binadamu kwa hulka yetu tunahitaji ishara ili tuamini jambo na ndio maana mara nyingi tuko tayari kusoma kwa bidii sana kwa sababu tunaamini kuwa mafanikio yetu kimaisha yanategemea elimu kubwa. Imani hii tumeipata kwa sababu tumemuona baba, mama, kaka dada au rafiki aliyefanikiwa katika masomo. Linapokuja swala la kufanya juhudi kubwa kuachana na vilema vyetu vya dhambi vinavyotusumbua ili tupate maisha ya raha mbinguni hadithi n itofauti na sababu kubwa ni kwamba kwa uhakika hatuna mfano tulioona wa mtu aliyefanya hivyo na sasa anapata raha mbinungi. Tumuombe Mungu atupe paji la imani tuweze kuamwamini Kristu pasipo kumgusa wala kumuona

No comments:

Post a Comment